Mkali wa RNB anaeiwakilisha Dodoma, Bernard Paul “Ben Poul” amedai yupo tayari kuipigia kura katiba inayopendekezwa ikiwa tu Maslahi ya wasanii yatahusishwa kwenye katiba hiyo.
Ben aliyazungumza hayo alipozungumza na Azam TV, mapema leo asubuhi akidai yeye si mfuatiliaji mzuri wa masuala ya kisiasa ila linapokuja kwenye maslahi ya kazi yake ni muhimu kuhusika kwenye harakati hizo.
“Mimi unajua sifatilii sana siasa, ila kuhusu katiba itabidi niseme jambo coz mimi kazi yangu inabidi iwemo mule, nitaangalia kwanza maslahi yangu mule kama yapo basi nitapiga kura, unajua ifike mahali hata mameneja wapate pesa ya kutosha kupitia huu huu mziki yani” alisema Ben poul
Pia alikiri hivi sasa ana menejimenti ambayo inamsimamia vizuri katika mziki, huku akiwataja Vanessa Mdee na Nah Reel kuwa chini ya menejimenti hiyo.
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.