Mwanamuziki na mtunzi wa nyimbo nchini Marekani Joni Mitchell amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi baada ya kukutwa akiwa amepoteza fahamu nyumbani kwake Jijini Los Angeles.
Mitchell alikimbizwa hospitali jana mchana saa za Marekani, na taarifa iliyotolewa kwenye tovuti yake imesema msanii huyo alirejewa na fahamu akiwa ndani ya gari la wagonjwa akielekea hospitali.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa mshindi huyo wa tuzo nane za Grammy, kwa sasa amelazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi akipatiwa matibabu na hali yake inaimarika.
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.