Mmoja kati ya wasanii washiriki wa filamu hiyo Kulwa Kikumba ‘Dude’ amedai kuwa sinema yao inaonyesha uwezo wa wakongwe katika tasnia ya filamu Swahilihood huku akijivunia aina ya uigizaji wa Waridi pamoja na wasanii wengine walioshiriki kutengeneza sinema ya Mchepuko.
“Msanii kama Waridi ni mwigizaji mwenye uwezo mkubwa na mwasisi wa fani ya uigizaji Bongo kwani kumbuka hawa ndio wasanii waliofungua njia kwa sisi sote ambao ndio tunaigiza filamu na tamthilia,”anasema Dude.
Filamu ya Mchepuko inawashirikisha wasanii kama Cathy Rupia, Dennis Sweya ‘Dino’, Waridi mwenyewe Kulwa Kikumba ‘Dude’ na wasanii wengine nyota kibao wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamu.