Google PlusRSS FeedEmail

THE GAME AINGILIA BIFU LA LIL WAYNE

Rapa kutoka nchini Marekani, The Game ameingilia kati bifu ya Lil Wayne na Young Thug kwa kumponda Thug na kumtetea Lil Wayne.

Jumanne mei 6,2015 The Game alisimamisha show yake kwa muda wa dakika kadhaa wakati akipafomu katika mji wa New Orlando, na kuongea maneno machafu yakimlenga Thug na kumuonya atamfanya kitu mbaya endapo kama ataendelea kumfuatafuata kwa maneno na kumdiss Wayne.

Ni miezi kadhaa sasa, Thug na Lil Wayne wamekua wakitupiana maneno ya vijembe kwa njia ya mitandao yao ya kijamii na kwenye kumbi mbalimbali za burudani wakati kila mmoja akifanya show.

Inasemekana kuwa chanzo cha ugomvi kati ya marapa Thug na Wayne ni kutokana Young Thug kuweza kurap kwa style ya Lil Wayne na kuteka soko la muziki huku Wayne akionekana kupotea kwenye ramani.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging