Google PlusRSS FeedEmail

YEMI ALADE MAHABA NIUE



Mtandao wa jaguada.com umeandika stori inayomuhusu mwanamuziki Yemi Eberechi Alade kutoka Nigeria aliweka wazi kwamba yupotayari kumkisi na kutoka na Chriss Brown kama mtu na mpenzi wake.

Yemi Alade ambeye ameshinda tuzo ya Mwanamuziki bora wa Afrika Magharibi kwa mwaka 2015 alisema, “Chriss Brown ni mtu ambaye sitokua na kipingamizi nae na nipotayari kulala nae na kufanya yetu kwenye kitanda kimoja”.

Pia alimtaja kama Mwanamuziki Beyonce kama rolemodel wake, huku akiwatetea wanamuziki wanaotoka na watu wao wa karibu wanaosimammia kazi zao mfano meneja na msanii akisema kwamba mapenzi ni maamuzi ya mtu hivyo si kitu cha ajabu.

Mwanamuziki huyo ambaye alitoka na wimbo wake wa John huku kwa sasa ngoma yake ya Kissing ikiendelea kufanya vizuri kwenye vyombo mbalimbali vya habari, pia alisema katika maisha yake ya kila siku anapenda sana kunywa maji, kula matunda na kutabasamu mara kwa mara.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging