Google PlusRSS FeedEmail

AMBER ROSE ATOA SIRI ZA MAFANIKIO



Kimwana wa zamani wa Kanye West na aliyekua Mama mtoto wa Rapa Wiz Khalifa, Amber Rose ametoa kitabu chake kinachotoa somo la jinsi ya kufanikiwa kwenye maisha,kikiandikwa na yeye mwenyewe huku kampuni ya Simon & Schuster Imprint ikisimamia mchongo mzima wa uchapishaji na usambazaji.

Kitabu hicho kinachoitwa “How To Be Bad Bitch” kitakua mtaani hivi karibuni na jumapili ya wiki iliyopita Amber Rose ameachia picha za Cover ya kitabu hicho kwenye akaunt yake ya Instagram.

Amber Rose amesema, Kitabu cha How To Be Bad Bitch, kitatoa elimu ya namna gani ya kufanikiwa katika maisha ya kila siku, hivyo amewataka watu wakinunue kwa wingi kitakapotoka rasmi.

Mara baada ya kutoa kava, tayari habari za kitabu hicho zimeshaanza kusambaa kutoka na picha za kava hilo likionyesha sehemu kubwa ya mwili ya How To Be Bad Bitch ikiwa wazi.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging