Staa aliyeimba wimbo huo Mwanadada, Mwasiti amejibu tuhuma za wale wote wanaodhania kwamba amepotezwa na wasanii wapya wa kike walioibuka kwenye game ya Bongo Flava.
“Kila mmoja ana ladha yake, na kila mmoja ananafasi yake, mimi nipo na nitaendelea kuwepo na hakuna anayenitisha”, Amefunguka Mwasiti,
Kuhusu kukaa muda mrefu kwa yeye baada ya kutoa ngoma moja, Mwasiti amesema huo ndio utaratibu wake kwani tangu 2009 enzi za wimbo wake wa Nalivua Pendo mpaka leo kila mwaka amekua na utaratibu wa kutoa single moja moja.
Mwasiti, hakusita kuwapa pongezi wanamuziki wapya wa kike walioibuka na kufanya vizuri huku akiwatahadharisha kuwa makini kwenye kazi zao.