“Mziki wetu umekuwa sana hivi sasa, kila mtu anafanya kwa uwezo wake”, hiyo ni kauli ya Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa akizungumza jijini Dar es Salaam.
Ni dhahiri kwamba “game” yetu imekuwa kwa asilimia kubwa hivi sasa, kwani hata ilipoonekana post ya Television kubwa Africa “MTV” kwenye Instagram, ikiongelea kuhusu kuachia nyimbo mpya ya Diamond “NANA” aliyomshirikisha MR Flava, haikushtua sana kwa maana ni kitu ambacho tunaelekea kukizoea hivi sasa.
Well wakati Plutnumz akifanya hayo, hasimu wake wa karibu “Ally kiba” ameshare picha kadhaa IG zikionyesha muda mwingi anautumia studio “Combination sound” kwa ajili ya kutuletea ngoma inayofuata baada ya Chekecha.
“Mzigo mwingine huo baada ya #chekecha #cheketuavideo #kingkiba” ameandika kupitia Instagram.
Hii ni ishara nzuri kwamba tunaendelea vizuri na tasnia hii, ambayo imeajiri vijana kwa asilimia kubwa nchini kwetu.
Swali? Unafikiri serikali imeweka mkazo katika kusimamia maslahi ya wasanii??
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.