Kwa mujibu wa mtandao wa habari New Orleans Times-Picayune, Polisi wa mji wa Eastern New Orleans wamethibitisha kumuona rapa Widner a/k/a Flow kuhusika kwenye tukio la mauaji la ndugu wawili Kenard na Kendrick Bishop, lililotokea may 25 mwaka huu.
Mili ya ndugu hao ilikutwa kwenye gari, vipande vya video kutoka kwenye kamera za usalama zilizotegeshwa katika eneo lililotokea mauaji vilimuonyesha Flow akitoka kwenye gari hilo pamoja na mwenzake ambaye hakuweza kufahamika.
Tayari polisi wametoa tangazo la kumsaka na kumkmata rapa huyo, huku wakiomba wanachi wenye taarifa zaidi kuhusu mauaji hayo wazitoe haraka ili uchunguzi uendelee kufanyika.
Rapa Flow alisaini mkataba na kampuni ya Lil Wayne “Young Money Entertainment” mwaka 2012 na habari zinaeleza kwamba sauti yake itasikika kwenye mixtape mpya ya Lil Wayne inayotarajiwa kutoka hivi karibuni.
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.