Google PlusRSS FeedEmail

SIPENDI MAMBO YA KIZUSHI - SNURA

                Snura Mushi
MWIGIZAJI wa filamu na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Snura Mushi ‘Mama wa Majanga’ amesema kuwa anakerwa sana na unafiki unaofanywa na baadhi ya wasanii kwa kushirikiana na wapenzi wa kazi zao kwa kufanya kampeni za kuangushana katika medani za kimataifa.

“Naepukana na unafiki tena naweza kusema roho mbaya chuki kwa baadhi ya wasanii kuunda makundi ambayo yantumia muda mwingi kuwadisi wengine, mfano hivi sasa wakati Diamond anagombea Tuzo kimataifa eti kuna watu wanaungana na watu wa nje kumfanya kampeni ashindwe,”anasema Snura.

Snura anadai kuwa siku hizi makundi ambayo yanaundwa na wasanii au wapenzi wenyewe ambayo yanatumika vibaya katika kutengeneza ugomvi, au kushabikia wasanii wakigombana kwa kutumia mitandao ya kijamii kuwatusi au kukatisha tamaa hata kama wanafanya kazi zinazotangaza Taifa.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging