“Naepukana na unafiki tena naweza kusema roho mbaya chuki kwa baadhi ya wasanii kuunda makundi ambayo yantumia muda mwingi kuwadisi wengine, mfano hivi sasa wakati Diamond anagombea Tuzo kimataifa eti kuna watu wanaungana na watu wa nje kumfanya kampeni ashindwe,”anasema Snura.
Snura anadai kuwa siku hizi makundi ambayo yanaundwa na wasanii au wapenzi wenyewe ambayo yanatumika vibaya katika kutengeneza ugomvi, au kushabikia wasanii wakigombana kwa kutumia mitandao ya kijamii kuwatusi au kukatisha tamaa hata kama wanafanya kazi zinazotangaza Taifa.