Google PlusRSS FeedEmail

BEN POL ATOA ONYO KWA WASANII WANAOJIINGIZA KATIKA VUGUVUGU LA KISIASA



Star wa RNB Bongo Ben Paul, amewataka wasanii wenzake kuacha ushabiki wa masuala ya vyama kama hawana uelewa mzuri wa siasa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Ben amedai kushangazwa na baadhi ya mastaa wenzie kuandika ‘post’ za kishabiki kwenye mitandao ya kijamii pasi na uelewa wa kile wanachokiandika.

“Mi nasema tu kama kweli wasanii vyama wanavyovishabikia wanavipenda kwa dhati haina shida, ila kama inafanyika kwa msikumo bila kuelewa ina madhara sana, wasikurupuke kuandika vitu ambavyo hawana uelewa navyo” alisema Ben Paul.

Kwenye ‘line’ nyingine, mkali huyo amemalizia kuwa haitaji kuhusishwa kwenye mijadala yoyote inayohusu siasa.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging