Dj huyo anayeendesha mambo yake kwenye mji mkuu wa Kenya Nairobi, anasema alishangazwa na tuzo hilo licha ya yeye kuwa maarufu katika nyanja ya muziki tu.
Makena ambaye alikuwa akiigiza kama, Didi the unlucky, ambaye ni mwanamke aliye na hamu ya kupendwa, alitangazwa kuwa mshindi kwenye sherehe zilizoandaliwa katika ukumbi wa Orpheum, jimbo la California nchini Marekani mnamo tarehe 12 mwezi huu.
Makena alielezea furaha yake baada ya ushindi huo na kuandika kwenyr mtandao wa Instagram akisema kuwa, Mabibi na Mabwana, Nimeshinda! Nimeshinda! Nimeshinda!