RAPPER ATOA USHAURI KWA WATUMIAJI WA MITANDAO
Rapper wa Marekani mwenye Hits za kutosha The game, ametoa ushauri kwa rappers wenzie na fans kwa ujumla juu ya matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii.
The game anayejulikana kwa kujibizana na mashabiki wake mara kwa mara mitandaoni, amedai binafsi yeye haruhusu mitandao kumuendesha bali huwa akiiendesha yeye.
“Mitandao ya kijamii ukiitumia vizuri unafanikiwa, ukiamua ikuendeshe basi utakuwa ukigombana na kila mtu, mimi huwa naitumia kama ‘platform’ ya muziki wangu” alisema The game.