Google PlusRSS FeedEmail

MANENO YA ICE CUBE BAADA YA NWA KUTAJWA KUWANIA ROCK



Rapper Ice Cube ametoa tamko baada ya ‘Crew’ yao ya kitambo ya Hip Hop N.W.A, kutajwa kuwania tuzo za Rock & Roll hall of fame kwa mara ya pili.

Cube anasema anajisikia vizuri na faraja kuona mchango wa N.W.A, unatambuliwa na kuheshimika kwenye ulimwengu wa muziki.

“Ni kitu kikubwa kiukweli kwa mwaka huu, hii inatupa nguvu kila siku kuendelea kufanya vizuri, na hii ni moja kati ya kudumisha ndoto za Easy E” alisema Ice Cube.

Wengine waliotajwa kuwania kipengele kimoja na N.W.A ni Janet Jackson, Nine Inch Nails, the Smiths, Deep Purple, Chic, Steve Miller, Chicago, Chaka Khan, the Spinners, Cheap Trick, the Cars, the J.B.’s, Los Lobos na Yes.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging