Hatimaye wapenzi wa muziki wa kizazi kipya usiku wa tarehe 26 Machi waliweza kuthibitisha kuwa Malima Lawrence a.k.a Marlaw na Besta Rweyemamu ni wanandoa.....Katika hali ya sintofahamu MC wa shughuli ya utoaji tuzo hiyo Millard Hayo aliwaita jukwaani Bwana na bibi Marlaw ambao walipanda jukwaani kwa ajili ya kumtangaza msanii bora wa muziki wa hip hop
Marlaw alikuwa wa kwanza kuzungumza na kutaja kipengele kilichopo na hatimaye Besta kumalizia kuwa mshindi wa kipengele hicho ni Joh Makini huku ukumbi huo ukirindima kwa shangwe kubwa
Dah mwisho wa siku hawa jamaa ni mke na mume...Tuko pamoja??








