Google PlusRSS FeedEmail
Showing posts with label ABOUT PRO24. Show all posts
Showing posts with label ABOUT PRO24. Show all posts

Fani ya muziki inazidi kukua siku hadi siku kwa kuongezeka kwa idadi kubwa ya watu kujua muziki pamoja na kuufanya muziki kuwa sehemu yao ya maisha

Ukizungumzia tasnia ya muziki bila shaka utamzungumzia dj ambae kazi yao kubwa ni kuutambulisha muziki kwa jamii nzima inayotuzunguka, pamoja na kumtambulisha msanii wa muziki huo

Unapowataja ma Dj wa Pro 24,hauwezi kuliacha jina la 'Dj Dea' ambaye ni moja kati ya ma dj wanaokuja kwa kasi katika tasnia hiyo huku akiwa na mchango mkubwa katika kulinga'risha jina la Pro 24

Alex Ashery ndiyo jina alilopewa na wazazi wake, ila kutokana na msukumo mkubwa wa kazi na kuwa na kitambulisho kitakachomtambulisha yeye pamoja na kazi yake akajikuta anapewa jina la 'dJ-DEA'

DJ-Dea alianza kazi ya kuwa dj mnamo mwaka 2008 akiwa anapiga muziki katika kumbi mbalimbali ikiwemo Emma Entartainment

Dea alifanya kazi hiyo sehemu tofauti tofauti kwa takribani miaka 4 ndipo alipojiunga na kundi zima la Pro 24 dj's Anasema kuwa alivutiwa na kundi hilo la Pro 24 kwa kile kitendo cha wao kama kundi kufanya kazi kwa ushirikiano wa hali ya juu huku wakiwa na nia moja ya kufika katika ngazi ya kimataifa tofauti na makundi mengine

Dea anasema kuwa mbali na ufanisi wa kazi pia  kikubwa kilichomfanya ajikute akisukumwa kujiunga na kundi hilo ni hile hali ya kutaka kupata nafasi ya kufanya kazi hiyo ya muziki katika hali iliyo kuwa  na mafanikio kwa kupata muongozo

Anasema kuwa mengi amejikuta akizidi kuyafahamu baada ya kuingia katika kundi hilo kwani hapo mwanzo alizoea kutumia mbinu za zamani ambazo sasa hazina nafasi katika soko la burudani

Anafunguka kwa kusema kuwa matarajio yake ni kuwa dj wa kimataifa, kwa kupitia kundi hilo atatimiza ndoto zake alizotarajia kwani ndani ya pro 24 ni chuo cha muziki kwake

Anaendelea kuelezea kuwa hauwezi kutarajia makubwa kisha ukabweteka, hivyo juhudi na kuongeza maarifa ndio kitu cha msingi ili uweze kufanikisha malengo yako

Dea anasema kuwa kikubwa wanachokifanya wao ni kufanya mazoezi ya kutosha kabla hawajafanya shoo hali hiyo inawajenga na kuwaongezea uwezo wa kujiamini na ujuzi wa kile wanachokifanya

Mbali na hilo mazoezi ni kitu ambacho kinawafanya kila siku kufahamu ni nyimbo gani mpya imetoka na ipi inafaa kupigwa katika kumbi za starehe 'Club' na zile zisizofaa kupigwa maeneo hayo,Anasema kuwa kwa kazi yao anakutana na changamoto kubwa, hususani kwao kwani sasa wanapiga nyimbo ambazo ziko kwenye mtindo wa video hivyo kila siku ni lazima waangalie ni video gani mpya iliyoingia katika fani hiyo

Dea ambaye amekili kuwa na mafanikio makubwa baada ya kuingia katika kundi hilo, akusita kutaja baadhi ya mafanikio yake yaliyotokana na pro 24 kwa kipindi kifupi tangu ajiunge hapo

Anasema sasa ameweza kuwa na uwezo wa kumiliki mashina yake ambayo inampa uhuru katika kuendeleza shughuri zake za muziki huku akiwa na uwezo wa kufanya mazoezi mahali popote

Mbali na hilo pia anasema kuwa kundi la Pro 24 Djs wanatumia vifaa vya kisasa ambavyo vinaendeshwa na komputa tofauti na makundi mengine ya ma dj, Anaeleza kuwa amekuwa na uwezo wa kutumia Techics Turntable System na Serato hivyo ni vifaa vya kisasa kabisa ambavyo vimemfanya kuwa na uwezo mkubwa na kukuza kipaji chake cha muziki na kufikia lengo la kuwa wa kimataifa

"Nimeachana na kutumia Cd kupiga muziki, dj wa ukweli unatumia Technics Turntable System na Serato hii inaonyesha ni jinsi gani ulivyokuwa na uwezo wa kucheza na mashine zenye hadhi ya kimataifa" alijinadi

Dea ambaye pia anapiga muziki sehemu mbalimbali za Club nchini Tanzania ingawa kwa sasa anapiga muziki katika kituo cha Terevisheni cha Taifa (TBC 1) kinachorushwa kila siku ya Alhamisi kuanzia saa 5 usiku huku akionekana kuwa mahiri katika ufunguzi wa shoo hiyo

Anaelezea kuwa yeye hupangwa katika ufunguzi wa shoo hiyo kwa kile kinachodaiwa uwezo wake na ubunifu wake kwa kuweza kuisoma hadhira yake

Anasema kuwa uwezo huo ameupata katika kundi hilo la pro 24 kwa kufanya mazoezi kwa bidi huku kila siku akifikilia kuongeza ubunifu ili awe na mvuto mkubwa katika kazi zake, Anaelezea kuwa anauwezo wa kufanya shoo kubwa za wasanii wanaokuja nchini kwa ajili ya kufanya shoo na wasanii wa hapa nyumbani

Dea ambaye ambaye mbali na kuwa dj yeye pia ni mcheza mpira ambaye anamudu kucheza namba 7 kama winga, Anasema kuwa mbali na kuwa dj pia yeye ni mcheza mpira mzuri ambapo anatumia muda wake wa mapumziko kwa kucheza mpira hali hiyo inamsababisha kujikinga na vishawishi ambavyo wanakutana navyo

Anasema kuwa anaheshimu kazi yake kwani inampatia kipato ambacho ndicho kinachomsaidia kuendesha maisha yake ya kila siku hivyo dj kwake ni kazi ambayo yeye anaheshimu

DJ DEA WA PRO 24 ANAJIVUNIA KUTUMIA TURNTABLE SYSTEM&SERATO

Fani ya muziki inazidi kukua siku hadi siku kwa kuongezeka kwa idadi kubwa ya watu kujua muziki pamoja na kuufanya muziki kuwa sehemu y... [Read More]


Dj Micho anaye 'wapagawisha' kila kukicha mashabiki wa muziki Tanzania kwa kuweza 'kuzidondosha' kwaito za kisasa na kusababisha mashabiki kucheza kwa 'step' huku wakienda sambamba na mapigo bila kukosea wala kuvuluga mtindo huo

Dj Micho ambaye ni mmoja wa ma Dj wa Pro-24 wanaotamba pwani ya Afrika Mashariki kwa 'kupagawishwa'mashabiki wa nyanja za muziki kwa kupiga vionjo vyote vya muziki vinavyopatikana Dunia kote

Dj Micho ambaye jina lake kamili ni Paschal Materego ni msomi wa Chuo cha Mipango Dodoma mwenye stashahada ya Mipango ya Maendeleo ambaye ndoto yake ni na mchango mkubwa kwenye jamii kwa kuwa na mipango endelevu ya kuondoa umasiki katika jamii inayomzunguka

Alianza safari yake ya Dj mwaka 2010 mkoani Dodoma katika Club ya NK ingawa hajasomea fani ya muziki lakini aliweza kumudu kupiga vionjo vyote kwa kile achodai kuwa fani ya muziki ipo kwenye damu

Alidumu ndani ya club hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja huku akiendelea na masomo yake kwa kuwa anapenda fani ya muziki aligawa muda wake vyema ili asivuruge muda wa masomo

Mwaka 2011 nyota yake ilinga'ra na kujiunga na kundi la ma Dj wenye lengo la kuwa wa kimataifa Pro-24 Djs ambapo yuko hadi sasa akiendelea kutoa burudani kwa mashabiki wake

Aliamua kujiunga na kundi hili la Pro 24 Dj ili kukuza fani yake kwani katika kundi hilo pia kuna mafunzo yanayotolewa kwa ma Dj ili kukuza na kuongeza ujuzi wa fani hiyo

Baada ya kuingia katika kundi hilo amejikuta amekuwa na uwezo na ubunifu mkubwa tofauti na alipokuwa awali hivyo anaushukuru uongozi mzima wa kundi hilo kwa kumuwezesha kufika hapo alipofika

Anasema kiwango chake kimeongezeka mara mbili hii inasababishwa na changamoto anazopata ndani ya kundi hilo, na ndio vitu ambavyo alikuwa anapenda kufanya kazi kama kundi ili kuweza kudumu katika fani hiyo kwa kufanya vitu vizuri

Anasema mbali na kupiga muziki ndani ya club mbalimbali sasa anauwezo wa kupiga muziki katika vyombo mbalimbali vya habari na kuongezea kuwa anaweza kutambua na kutofautisha aina ya muziki ya kupiga katika mazingira tofauti tofauti

"Pro-24 ni chuo cha kujifunza fani ya muziki kwa ma dj kwani nilivyofika na sasa ni tofauti nimejikuta najua mbinu nyingi za kujiboresha na kuonekana bora zaidi kutofautisha na dj mwingine" anasema Micho

Akizungumzia utofauti wa pro 24 Dj na ma Dj wengine anasema kuwa  wao wanafanya mazoezi na kuchambua muziki kabla hawajapanda kwa ajili ya shoo hali hiyo inawajenga kuijua hadhira hivyo kuhakikisha hadhira hiyo inafurahia kile walichokiandaa

Mbali na hilo pia wao wanatumia vifaa vya kisasa ambavyo vinamsababisha dj kuwa na umakini na kumuongezea uwezo wa kuwa katika ngazi ya kimataifa

Anasema kuwa kila dj kwenye kundi hilo anamiliki vifaa vya kupiga muziki hivyo ni rahisi kwao kufanya mazoezi kila wakati na ndio kikubwa kinachowatofautisha na madj wengine kwani wao wanaamini kuwa dj ni ajira hivyo ni lazima uheshimu ajira yako

Dj huyo anapenda kupiga muziki yenye radha tofauti tofauti amebobea katika miondoko ya Kwaito muziki wa asili ya South Afrika pamoja na muziki wa Bongo Fleva

Mbali na hiyo dj huyo anakitu tofauti kinachomtofautisha na mad Dj wengine kwa kuwa anapiga muziki huku na yeye akicheza miondoko ya muziki huo anaoupiga

Alipoulizwa kwa nini anapenda kucheza wakatia anapiga muziki anasema kuwa "ni mzuka ndio unapanda na ninapokuwa ninacheza ndio nazidi kuwaburudisha mashabiki kwa kuchagua muziki unaoendana na mahari hapo na aina ya mashabiki ambao wapo katika mazingira hayo" anasema

Pamoja na hayo Dj Micho ambaye pia anapiga shoo kubwa za wasanii mbalimbali wanaotoka nchi tofauti anasema kuwa hali hiyo inamsababisha kila siku afikilie kitu tofauti yaani kuwa mbunifu

Anasema tangu alipojiunga na kundi hilo amepata mafanikio makubwa mbali na kuongeza ujuzi pia ameweza kujiendeleza kimaisha

Mbali na kuwa Dj pia ni shabiki mzuri wa timu ya Manchesta huku akiwa anapenda sana kula chakula cha aina yeyote kila ilimradi tu kiwe kimepikwa katika mazingira mazuri

Kwa upande wake yeye hatumia kinywaji chenye kileo chochote kile hii inamjenga kuwa makini kwenye kazi zake na kufikilia kila siku nini afanye ili awe bora

Dj Micho anasema kuwa kazi yao inachangamoto kubwa sana hususani kwenye vishawishi vya kujiingiza katika vitendo vya ngona na wanawake tofauti tofauti

Anaelezea kuwa yeye anajitahidi kupambana na changamoto hizo kwa kuwa na mpenzi mmoja ambaye wanaaminiana na wakati mwingine kuwa naye hata sehemu yake ya kazi ili kuzibitisha kuwa yuko salaama na muaminifu kwa mwenza wake

DJ MICHO MTAALAMU WA 'KUGONGA MIONDOKO' YA KWAITO

Dj Micho anaye 'wapagawisha' kila kukicha mashabiki wa muziki Tanzania kwa kuweza 'kuzidondosha' kwaito za kisasa na kusa... [Read More]









Miaka ya nyuma baadhi ya watu walikuwa wanaamini kuwa Yule anayepiga muziki au kwa jina linalofaamika sana ‘DJ ‘ katika ukumbi za starehe usiku maalufu kama ‘Disko’ ni muhuni na hana elimu ya kutosha

DJ K-Flip ni mmoja wa kundi la Madj wa Pro -24 ambaye yeye anaonyesha utofauti wa dhana hiyo waliyonayo baadhi ya wanajamii kuhusiana na madj kuwa wahuni pamoja na kukosa elimu

DJ K-Flip jina lake Halisi Calvin Michael "DJ K-Flip" likiwa linamtambulisha kazi yake anayoifanya kwa mashabiki wake wote ndani na nje ya nchi, akielezea safari yake ya kuwa DJ alisema kuwa alianza kazi hiyo mwaka 2006 kwa kuajiliwa kupiga muziki Club pamoja na Radio ijini Arusha

Club ambazo alifanya nazo kazi jijini huko ni pamoja na Triple A,Club AQ na  huku akiugawa muda wake kwa kuwahakikisha anatoa burudani kwa mashabiki wake wote kwa kutumia radio ya Triple A

Alifanya kazi jijini hapo takribani miaka minne ndipo alipoamua kujiunga na kundi la madj wa Pro 24 huku akiwa na ndoto lukuki za kufanya kazi kama team ili aweze kukabiliana na changamoto

“Kilichonisukuma kujiunga na kundi hilo ni kwa sababu nilikuwa napenda kufanya kazi kama ‘Team’ kundi kwani kwa kufanya kazi kwa kushirikiana unaongeza ujuzi na pia kunakuwa na chanagamoto ambazo ukizitumia zina kuinua kiwango “ alisema Calvin

Calvin alisema baada ya kujiunga katika kundi hilo amepata mabadiliko makubwa kwa kuongeza ujuzi siku hadi siku kwa kuwa ndani ya kundi hilo kuna mafunzo ambayo yanatolewa kwa ajili ya kuboresha ujuzi

Akizungumzia kundi hilo la Pro-24 Dj’s anasema kuwa ni kundi ambalo lina mategemeo ya kusaidia vijana hususani wenye kipaji cha kuwa Dj kwa kutoa mafunzo yatakayo msababisha Dj kuujua muziki na kujua ni aina gani ya muziki upige kulingana na mazingira yaliyopo

Anasema tangu alipojiunga na kundi hilo amekuwa akipiga muziki sehemu mbalimbali hali hiyo imemsababisha kujiongezea mashabiki wengi ambao wengi wao wameonekana kupenda kazi yake anayoifanya

Kwa hivi sasa Dj huyo anapiga sehemu tofauti tofauti zikiwemo Club Bilicans, Maisha , Masai , Savannah Lounge jijini Dar es Salaam ingawa pia anapiga katika mikoa mbalimbali pale anapohitajika kufanya hivyo hii yote ni kwa ajili ya kuwapa radha mashabiki Tanzania nzima

Anasema kuwa amekuwa na tofauti kubwa kabla ya kujiunga na kundi hilo kwani hapo mwanzo alikuwa ni Dj wa Club pamoja na Radio, wakati sasa ni tofauti amekuwa akifanya vipi tofauti tofauti kwenye televisheni

DJ K-Flip pia amekuwa akifanya shoo katika vipindi vya televisheni tofauti tofauti huku akiongezewa ujuzi na kundi hilo la Pro- 24 kwani nia yao ni kutoa burudani kwa mashabiki wao

Anafanya shoo ndani ya Clouds TV katika kipindi kinachojulikana D'Wikend Chat-Show kinachorushwa kila siku ya Ijumaa, pia anafanya shoo katika Terevisheni ya Taifa (TBC 1) kinachorushwa kila siku ya Alhamisi kikiwa kinadondoshwa na kundi zima la Pro 24

Dj K-Flip anakubali kupata usumbufu kutoka kwa mashabiki wake lakini kwa kuwa anajali kazi yake na ili asiwapoteze mashabiki wake anaamini kuheshimu kile anachokifanya kwa kumuheshimu kila shabiki na kufuata maadili ya kazi yake

Anasema kuwa msingi mkubwa wa kukwepa vishawishi ni kufuata maadili ya kazi ikiwemo kuheshimu sehemu ya kazi ili uweze kufikisha kile unachokikusudia kwa jamii nzima bila ya kupoteza maadili ya kazi pamoja na nchi

Anaongezea kuwa kazi ya DJ si ya kiuni kama watu wanavyofikilia, kwa upande wao anasema kuwa kwao ni ajila na wanaheshimu ajila hiyo kwa sababu wanapata kipato na kuendeleza maisha yao kutokana na kile wanachokifanya

Calvin anaeleza kuwa kunatofauti ya mashabiki, akizungumzia utofauti huo anasema kuwa mashabiki wa Club hawajamsababishia madhara tofauti na mashabiki wa televisheni kwani wamekuwa mtaani kwa sababu wanamuona akiwa anafanya shoo hizo

Calvin anajinadi kwa kusema kuwa kila siku anawaza kufanya bora zaidi ya mwenzake kwa kuhakikisha hilo anapokuwa anafanya shoo anahakikisha kuwa kila shabiki anafurahia kile anachokipiga

“Nikipanda kwenye shoo naingia na mzuka kwa kupiga misumari ili kusababisha mizuka kwa mashabiki wangu na wakubali kile nianchokifanya “ anasema

Mbali ya kuwa Dj,pia ni mwanafunzi wa chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM )akiwa anasomea shahada ya Fedha na Uchumi huku akiwa na ndoto lukuki za kuwa mchumi katika nchi yetu

Calvin alisema kuwa kazi yake hiyo ya Dj haiaribu ratiba yake ya masomo na cha zaidi anahakikisha anasoma kwa bidi ili aweze kufanya vizuri pamoja na kutimiza ndoto zake

Calvin anapenda sana kuchati na marafiki wa jinsi zote , hatumii kinywaji chenye kilevi chochote kwani anaamini kwa kutumia kilevi utakuwa unajiingiza katika vishawishi vingi hivyo anapendelea zaidi kunywa juice na maji





DJ K-FLIP MWENYE SHAHADA YA FEDHA NA UCHUMI ALIYEBOBEA KATIKA MASWALA YA MUZIKI

Miaka ya nyuma baadhi ya watu walikuwa wanaamini kuwa Yule anayepiga muziki au kwa jina linalofaamika sana ‘DJ ‘ katika ukumbi... [Read More]

About Pro24

[Read More]

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging