Mwimbaji Diana Samkange amefungua studio kwa lengo la kuibua wasanii wapya katika tasnia hiyo ya muziki ambayo kwa sasa ni ajira kwa dunia nzima
Studio hiyo ambayo ameipa jina la Mangwenya imekuja baada ya kumaliza kozi yake ya kujifunza kupiga kifaa cha muziki kiitwacho Mbira
Alisema kuwa kilichomfanya kufungua studio hiyo ni kumbukumbu alikotoka kwa kuwa waandaaji wengi wanasahau ulipotoka na kuwaacha wasanii wachanga wahangaike bila kuwaunga mkono