Wakati Rappers Jay Z na Eminem wakiwa katika show za pamoja katika baadhi ya states za huko Nchini Marekani..
Katika kuwaweka mashabiki katika hali ya furaha zaidi Wanamuziki hao wawili kwa pamoja wamefanya bonge la surprise baada ya kuwaalika wasanii wenzao kuwapa shavu bila ya kutoa taharifa kwa mashabiki wao,kati ya waliokuwepo katika surprise hiyo kwa ajili ya mashabiki ni Nicki Minaj, Kanye West, 50 Cent vile vile Dr. Dre and D12 walionekana wakiwa wanasaidia wahusika wa show hiyo katika baadhi ya mashairi katika nyimbo zao ambazo walikuwa wakiziimba kwa ajili ya kuwatumbuiza mashabiki wao...
Show hiyo imekuwa na msisimko nchini marekani baada ya watu wengi hawakutegemea wasanii hao wote wangeimba kwenye stage moja,na kikubwa kimewashangaza kutokana na kutopewa taharifa kwamba kungekuwa na wasanii wengine wameongezeka...
Jay-Z katika ukurasa wake wa twitter amesema lilikuwa wazo lake na alifanya hivyo kwa ajili ya mashabiki wote wa kwake na wa Eminem...








