Michael alifariki dunia mnamo June 25 mwaka 2009 na tangu kifo chake tayari kuna baadhi ya nyimbo zake zimeanza kuachiwa hewani,,kama utakumbuka Michael mpaka kifo chake, alikuwa katika mazoezi mazito kwa ajili ya uzinduzi wa albamu yake mpya ambayo alitarajiwa angeizindua kwa mara ya kwanza nchini Uingereza,
Miezi miwili kabla ya show hiyo tayari tiketi za show hiyo zilikuwa zimeshamalizika..
Tayari ngoma mbili zimetoka rasmi wiki hii ambazo nazo zilikuwa katika albamu yake hiyo mpya..ngoma zilizotoka ni 'Blue Gangsta' and 'All I Need' ambazo zimeshaanza kuchezwa katika vituo mbali mbali vya radio duniani kote
Cha kushangaza kuna baadhi ya web zinasema kuwa nyimbo hizo zimeleak,zimetoka bila idhini ya waliokuwa na hakimiliki ya kuzipeleka hewani..








