Google PlusRSS FeedEmail

BONGO KUPIGA HATUA KATIKA TANSIA YA FILAMU

  Evans Bukuku,Karabani, Sauda Simba
Mratibu wa Filamu ya CPU, Bw Evans Bukuku amesema kuwa Filamu hiyo inalenga kuburudisha na kuelemisha jamii kwa ujumla. ikiwa imechezwa hapa hapa Dar es salaam katika maeneo tofauti ya jiji, ili kuleta uhalisia zaidi. Filamu ya CPU ni mwanzo wa mapinduzi makubwa ya kihistoria katika tasnia ya filamu hapa Tanzania na Afrika. Ikiwa imetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu katika Picha, sauti, uigizaji kiujumla kila kilichofanyika ndani ya CPU kimefanywa kwa umakini na utashi wa aina yake. Mpaka sasa tunaweza kusema CPU ni miongoni mwa Filamu chache sana zilizoweza kutengenezwa kwa ubora wa hali ya juu hapa Afrika.
            Helcopiter
                                       Timu ya CPU ikijiandaa kupaa angani na Helkopita.

CPU Ni aina ya filamu ya kipelelezi yaani “Investigatory story” ikiwa inazungumzia kitengo kilichoundwa kwa ajili ya kufuatilia na kutatua matatizo mbali mbali wakati jukumu lao la kwanza ni kufuatilia juu ya mtoto mchanga aliyeokotwa pasipo kufahamika ni wa nani. Hivyo Maria Isabela (Sauda Simba) anateuliwa na serikali kuongoza timu hiyo, katika hilo inabidi awashawishi watakao msaidia ambao ni Alex Kibera(Nkwabi Juma) jambazi suguanayetumikia kifungo cha miaka 30 jela, David Kifati(steven Sandhu) mtaalamu wa kompyuta na kijana mwenye uelewa mkubwa ambaye anatoka katika familia bora na anayependa anasa.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging