Google PlusRSS FeedEmail

UPENDO NKONE KUSHIRIKI KATIKA TAMASHA LA PASAKA

Upendo Nkone anatarajiwa kuwa miongoni mwa waimbaji watakaopamba tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika Aprili 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mratibu wa tamasha hilo, Alex Msama wa Kampuni ya Msama Promotions, alisema Dar es Salaam jana kuwa Nkone amekuwa mwimbaji wa pili kuthibitisha kushiriki tamasha hilo baada ya Upendo Kilahiro. Tamasha hilo la aina yake, baada ya kufanyika Dar es Salaam, pia litarindima kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 9 mwaka huu. Tamasha la Pasaka mwaka huu malengo yake makubwa ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji wanawake wajane.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging