Google PlusRSS FeedEmail

AUNT EZEKIEL KUFUNDWA MWEZI UJAO



Msanii mwenye jina na asiyeisha vituko, Aunt Ezekiel anatarajiwa kufundwa Oktoba 24, mwaka huu ikiwa ni maandalisi ya harusi yake inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni

Aunt Ezekiel ambaye kwa sasa inadaiwa hapikiki na wakwe zake , amekana hilo na kudai anapendwa kama 'Ubwabwa kwa njegere'na ndio maana atafundwa siku hiyo

'Shuhuli' ya kumfunda inatarajiwa kufanyika ndani ya Milimani City kabla ya wiki moja baadaye kufanyiwa sherehe katika hoteli ya Serena

Kuhusu kukataliwa ukweni, Aunt Ezekiel amedai taarifa hizo hazina ukweli wowote kwani anaamini watu wenye chuki zao ndio wanaosambaza uongo huo ili kumuharibia mambo yake

Alisema mpaka sasa taratibu za harusi yake zinaendelea kwa ushirikiano mkubwa wa wakwe zake na mume wake mtarajiwa aitwaye Demonte.
Haya yamekuja huku Aunt Ezekiel akiwa 'amechafuka' kutokana na picha zake za uchi kusambaa katika mitandao mbalimbali

Mwenyewe amekiri hilo na kudai kuwa wakati akifanya kitendo hiko alikuwa hajielewi kutokana na kuzidiwa na kilevi

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging