WASANII WA FILAMU WAJIUNGA NA NSSF
Wasanii zaidi ya 200 kutoka Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) wamejiunga na Shirikala Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),baada ya kuvutiwa na shirika hilo
Akizungumza na wasanii hao Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NSSF ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika hilo, Cresentius Magori, alisema wasanii hao watafaidika na mafao saba
Magori amewaita wasanii hao ni wajanja kwa kujiunga na NSSF, shirika ambalo amedai linauwezo mkubwa kiuchumi hivyo watafaidika kwa kuuziwa nyumba zinazojengwa kwa masharti nafuu na kupata matibabu bure
Naye Rais wa TAFF, Simon Mwakifambwa alitumia nafasi hiyo ya kuwashukuru NSSF na kuahidi kuwa watapita nchi nzima kuhamasisha wasanii wengine kujiunga na NSSF
Baadhi ya wasanii maarufu waliojiunga na NSSF ni Steven Jacob 'JB', sEIF mBEMBE, Maghfidh Awazi 'Dkt. Chen', Keti Rupia,Steven Nyerere, Salome Nong na Kojaki