Google PlusRSS FeedEmail

BAADHI YA 'MAPRODUCER' NCHINI WANACHORA




IMEELEZWA kuwa sababu zinazosababisha kufanana kwa kazi za muziki hususani wa kizazi kipya ni kuitokana na maproducer kushindwa kupiga kinanda 'live' na matokeo yake wanachora mtindo wa midundo wanayoitaka kwa kutumia komputar

Hayo yalielezwa na Producer anayekuja kwa kasi kwa kutengeneza nyimbo zinazofanya vizuri Afrika Mashariki Emanuel Maungu 'E.M.A theboy' alipokuwa akielezea sababu zinazosababishwa kuwa na mfanano wa kazi za muziki wa bongofleva

Alisema tatizo liko kwa maproducer ambao ni wavivu wasiotaka kubadilika na kusoma muziki hivyo wanashindwa kutumia vifaa ili kutengeneza muziki ulio na ubora zaidi

Alileza kuwa tatizo la kuwa na kufanana kwa kazi hiyo inatokana na maproducer kushindwa kutumia kinanda hivyo wanategemea komputar pekee kutengeneza muziki wakati wanatakiwa kujua kupiga kinanda 'live' alafu ndio utengeneze muziki kwenye komputar

"Tatizo maproducer wengi wanachora sababu ambayo inachangia kupata muziki unaofanana na kukosa ladha ya muziki kwani kwa kutojua kinanda huwezi kupiga vitu vingi, pia inachangia kutumia muda mrefu kutengeneza muziki" alisema E.M.A theboy

Mbali na hayo pia aliongezea kuwa baadhi ya wasanii pia hawajui kuimba na hawataki kujifunza hivyo matokeo yake kila siku kinaimba kitu kile kile na kupoteza ladha kabisa ya muziki wa bongofleva

E.M.A theboy ni producer amabye teyari ameshatengeneza nyimbo zinazofanya vizuri katika sekta ya muziki huu wa bongofleva nyimbo kama 'Sory' aliyoimba Barnaba, Upepo iliyoimbwa na Recho, 'Me anda you' iliyoimbwa na Ommy Dimpozi







This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging