Google PlusRSS FeedEmail

BBA THE CHASE: FEZA AINGIA DANGER ZONE, HURUMA YA WATANZANIA WATAKAOMPIGIA NDIO ITAKAYOMUOKOA.




JUMATATU asubuhi katika jumba la Big Brother ilikuwa ni siku ya washiriki kupendekeza majina ya washiriki ambao wangeingia katika Danger Zone. Katika la jumba la Ruby washiriki Biguesas wa Angola na LK4 wa Uganda ndio aliopata kura nyingi zaidi kutoka kwa washiriki wenzao kwenye jumba hilo, ambapo kama kawaida kiranja wa jumba hilo au HOH ana nafasi ya kumuokoa mmoja kati ya hayo na kumuweka mwingine. Katika chumba cha mahojiano (Diary room), mshiriki kutoka Ghana Selly ambaye ndio HOH wa Ruby alimuokoa Biguesas na baada ya kufikiri kwa muda akamtaja Koketso kuchukua nafasi ya aliyemuokoa, hivyo hiyo inamaanisha kuwa washiriki watakaopigiwa kura na watazamaji katika jumba la Ruby watakuwa ni LK4 na Koketso. 
Kwa upande wa jumba la Diamond washiriki waliopigiwa kura nyingi kuingia kwenye Danger Zone na wenzao walikuwa ni Bolt wa Sierra Lione, Dillish wa Namibia na Hakeem wa Zimbabwe ambapo kama kawaida HOH huku nako pia alipata nafasi ya kumuokoa mmoja na kumbadilisha na mwingine. Katika chumba cha mahojiano HOH wa jumba la Diamond Betty kutoka Ethiopia alilipa kisasi kwa kumuokoa Bolt na kumuweka Feza ambaye ni mshiriki kutoka Tanzania katika Danger Zone. Kama utakumbuka Feza wiki iliyopita wakati akiwa HOH naye alimuokoa mmoja wa washiriki na kumuweka Betty.



Kwa maana hiyo washiriki Dillish, Hakeem na Feza ndio watakaopigiwa kura wiki hii, hivyo chonde chonde watanzania tujitahidi kumpigia kura mshiriki wetu Feza aendelee kubakia huko.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging