Google PlusRSS FeedEmail

LULU AKANUSHA KUCHUMBIWA


MSANII wa filamu nchini Elizabeth Michael 'Lulu' akanusha taalifa za kuzushiwa za kuchumbiwa na kukalibia kuolewa muda mchache zilizoandikwa na moja ya chombo cha habari jijini.

Lulu amekanusha taarifa hizo ambazo zimeandikwa na gazeti moja la udaku kuwa anatarajia kuolewa hivi karibuni  huku wazazi wake wakiwa tayari wameshapokea mahali.

Akizungumza na katika mahojiano katika kipindi cha XXL, muigizaji huo ameweka wazi kuwa ameshangazwa na habari hizo ambapo baadhi ya magazeti mengi ya udaku ndiyo yamekuwa yakimwandika kile wanachojisikia.

Aliweka wazi kuwa hajachumbiwa na mwanaume yoyote yule na siku ikitokea amechumbiwa basi kila mtu atajua kwani halitakuwa jambo la kificho tena.

"Sijajua wao wameipata wapi hiyo habari kutoka chanzo kipi, kila kukicha kumekuwa na habari mtu akijisikia kuandika tu anaandika bila hata ya kufikiria leo wameandika nimechumbiwa, kesho wataandika nimeolewa, tena wataandika nimeachwa, kila watakalo lihisi kuandika wanaandika" alieleza Lulu.

Aliweka wazi kuwa kuchumbiwa kuolewa ni vitu ambavyo vimeumbiwa binadamu, vipo kama ukiwa na mpango wa mwenyezi mungu nitachumbiwa.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging