CHAMA cha waigizaji TDFAA Taifa kimetangaza uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi zilizowazi kwa kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, ameeeleza mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Michael Sangu ‘Mike’ na kusisitiza wanachama hai wote kujitokeza na kugombea nafasi hizo kama zilivyotangazwa.Tunatangaza uchaguzi mdogo kwa mujiba wa katiba yetu ya TDFAA, ambao unatarajia kufanyika tarehe 11/January/2014, nafasi zinazotakiwa kujazwa ni wajumbe wane wa Bodi na tayari maandalizi yamekamilika kila mwanachama mwenye sifa za uongozi ajitokeze kugombea,”anasema Mike.
Fomu za wagombea zinapatikana katika ukumbi wa CCM Mwinyijuma Mwananyamala kwa gharama ya Tshs. 10,000/ tu, na mwisho wa kuchukua fomu itakuwa tarehe 07.January. 2014 mwenyekiti anasisitiza kufika kuchukua fomu hizo ili kujenga tasnia bora kwa kuwa na viongozi bora.