Tuzo za muziki Tanzania, (Kilimanjaro Music Awards) zimezinduliwa leo jijini Dar es Salaam ambapo watanzania wamepewa nafasi ya kupendekeza majina ya waimbaji watakaowania vipengele 34 vinavyoshindanishwa.
Akizungumza katika uzinduzi huo meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe amesema kuwa tuzo hizo zinakuwa kila mwaka hali inayoonesha kuwa kukubalika kwa tuzo hizo.








