Google PlusRSS FeedEmail

CHRIS BROWN 'ATAPATAPA' KURUDIANA NA RIHANNA

Mwanamuziki maarufu nchini Marekani, Chris Brown inadaiwa kuwa ameachana na mpenzi wake wa sasa Karrauche na kuamua kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Rihanna.

Chris  ameripotiwa kumbwaga mpenzi wake Karrauche huku akidaiwa kutaka kurudiana na mpenzi wake wa zamani, Rihanna. 

Ripoti zinasema kuwa hii ilitokana na wivu ambao Chris ameshindwa kujizua kwa wasiwasi kuwa Rihanna sasa anarudiana na Drake ambaye ni adui yake mkubwa.

Mtandao wa Rada online umeripoti kwamba Chris alianza kumtumia Rihanna ujumbe wa simu kuanzia tarehe 20 februari, ambapo ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa na ndipo Karrauche alipoanza kuweka jumbe hizo katika mtandao wa Instagram na twitter, na kuacha kumfuata Rihanna katika mitandao ya kijamii.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging