Google PlusRSS FeedEmail

LUPITA ASHINDA TUZO YA OSCAR




MUIGIZAJI wa kike kutoka nchini Kenya, Lupita Nyong'o ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Oscar katika kipengele cha muigizaji bora msaidizi wa kike ambapo filamu ya utumwa '12 years a salve 'ndiyo iliyompa ushindi huo.

Hali hiyo ilitarajiwa na mashabiki wengi muigizaji huyo wa kike kunyakua tuzo hiyo kama muigizaji msaidizi wa kike aliyekuwa na jukumu lake alivyovaa uhusika wa Patseh katika filamu hiyo ya utumwa.

Baada ya kupokea tuzo hilo lupita amesema " Haikwepi katika mawazo yangu kwamba hata dakika moja ya furaha katika maisha yangu ni shukrani na maumivu makubwa kwa mtu mwingine.''

Kisha Lupita akaongeza kusema, " Na iwe ukumbusho kwangu na kila mtoto kwamba kokote unakotoka, ndoto zako ni halisi.''

Sherehe ya kutolewa kwa tuzo hizo zimefanyika mjini Los Angeles nchini Marekani.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging