“Nilikuwa nimesaini mkataba na Kundi la Vituko Show lakini kwasasa mkataba umekwisha nafanya kazi zangu mwenyewe sijabahatika kupata kampuni ya kufanya nao kazi,siyo kama sito rudi kwenye kundi langu la zamani naweza kurudi lakini kwa sasa ngoja nifanye kazi zangu mpaka nitakapo pata kampuni nyingine ya kufanya nayo kazi.
“Mfano sasahivi nipo Dar es Salaam kunakipindi natengeneza kinahusiana na katiba kitakua kinachekesha lakini kinaelimisha na ndiyo maana nikasema watu wasije wakahofia kuwa wakinihitaji kufanya kazi na mimi nitakataa,”anasema Masele.
Msanii huyo amesema kuwa hapo awali ilikuwa ngumu kufanya hivyo kwani alikuwa chini ya Al- Riyamy Production, kwa sasa yupo free kufanya kazi na msanii au kampuni yoyote itakayomhitaji.