“Ninapowaambia nimeokoka watu wanaangalia nywele zangu au viatu vyangu, lakini wamesahau Samson alikuwa vipi? Sasa nakuja na Street Gospel Ministry nitahubiri mtaa kwa mtaa iwe kwa Bajaji au Bodaboda,”
“Siku hizi Makanisa ni mengi kama vibanda vya M pesa lakini watu wamekuwa wagumu kumwabudu Mungu sasa nawaletea huduma walipo mimi Mchungaji Masanja,”anasema Masanja.
Msanii huyo anadai kuwa atawafuata Kondoo walipo ili kuwachunga, na mahubiri yake atayarekodi na kutengeneza video kwa ajili ya kuwapatia wale wanaotingwa na mambo ya Kidunia ili wapate kumujua Mungu.