Google PlusRSS FeedEmail

PROFESA JAY AFUNGUA WEBSITE YAKE

The heavy Weight MC, Profesa Jay ameanzisha website yake binafsi (official website) ambayo ina matukio mengi yanayohusu harakati ya muziki wake, nyimbo na video zote zinazomhusu.

Akiongea na Bongo Dot Home ya 100.5 Times Fm, Profesa Jay amesema kuwa ameamua kufanya hivyo baada ya kuona hitaji la kwenda na wakati na kwamba watu wengi hata walioko nje ya mipaka ya nchi wanataka kufahamu mwenendo wa muziki wake hivyo ameona ni vyema kuwapa sehemu ya kuvipata muda wowote.

“Nimeamua kuwa na website yangu kuzidi kujitengeneza, kujipackage na mtu aweze kukufikia kirahisi. Nimeona value yangu na nimeona wapi nilikosea, kwa muda mrefu watu wemekuwa wakiulizia website, kazi zangu watazipata wapi, wapi muziki wangu, wapi shows zangu…so kwenye website kutakuwa kuna kila kitu kitakachojiele. So kila kitu ntakachokuwa nafanya kitakuwa kinapatikana kwenye website yangu.” Amesema.

Katika hatua nyingine, profesa amesema kuwa atazindua video mbili za nyimbo zake ‘Kipi Sijasikia na Tatu Chafu’ pamoja na website yake Wikendi hii.

“Watu wakae tayari, kutakuwa na performance pale. Profesa Jay atakuwa anaperform, marafiki wangu ambao wananisapoti na tunasapotiana watakuwepo. Mastaa wengi pia watakuwepo kuona Profesa Jay amefanya nini. Kwa hiyo watu wakae tayari tutawapa information zaidi. Lakini by next week kama Ijumaa tutakuwa tunafanya uzinduzi.”

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging