Mshiriki wa Tanzania anayewakilisha ndani ya mjengo wa Big Brother ‘hotshots’ , Idris Sultan ndiye ameibuka kidedea leo usiku katika shindano hilo huko Afrika Kusini. Idris amekuwa Mtanzania wa pili kushinda shindano hilo, baada ya Richard Bezuidenhout kuibuka kidedea mwaka 2011 katika Big Brother Afrika II.
Ushindi huo wa Idris umeongeza heshima ya Tanzania hasa katika swala la burudani,mara baada ya Diamond kushinda tuzo 3 za channel o na moja kutoka Nchini Nigeria