Google PlusRSS FeedEmail

TICO APOKELEWA KISHUJAA

       
Mtayarishaji wa filamu Timothy Conrad ‘Tico’ ameingia leo kutoka nchini Marekani kwa alikoshinda tuzo ya filamu ya Dogo Masai kama filamu bora ya kiafrika tuzo zilizotolewa na za Silcon Valley African Film Festival (SVAFF) kama Filamu Bora kutengenezwa Afrika (The best African Production Movie ) tuzo hizi zilitolewa California Marekani.

“Nimefurahi sana kwa mapokezi haya hapa Uwanja wa Ndege kutoka kwa wasanii wenzangu wadau wa filamu na Familia yangu sina cha kuwalipa kwa moyo wao lakini Mungu atawalipa na kuwaongeza kilichopungua asanteni,”anasema Tico.

         
Baada ya kuondoka katika viwanja vya ndege vya Mwl. Nyerere aliekea moja kwa moja katika ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa alipata nafasi ya kuongea na wanaahabari na viongozi wa Basata kwa kushukru ushindi huo kwa kulitangaza Taifa la Tanzania.

“Tunapaswa kufanya kazi zenye ubora zinazoweza kututangaza na si bora kazi tunajivunia pale mtu anapovuka mipaka ya Taifa, tunafurahia kupokea tuzo kutoka Marekani,” anasema Agness msemaji wa Basata.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging