Gauni lenye thamani ya dola 150,000 sawa na shilingi milioni 270 za Tanzania alilovaa muigizaji filamu wa kimataifa Lupita Nyong'o mwenye asili ya Kenya kwenye hafla ya utoaji tuzo za Oscars limeibiwa katika chumba cha hoteli huko Hollywood.
Gauni hilo lililobuniwa na Calvin Klein Collection na mbunifu Francisco Costa lina vito vyeupe vya asili, lilichukuliwa kwenye hoteli ya London Magharibi mwa Hollywood, wakati Lupita akiwa nje ya chumba chake.
Muigizaji huyo ambaye baba yake ni mwanasiasa maarufu nchini Kenya, mwaka jana alishinda tuzo ya muigizaji bora msaidizi kwa ushiriki wake kwenye filamu ya Twelve Years a Slave na siku ya jumapili alitoa tuzo ya Oscars akiwa amevalia gauni hilo.
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.