Mwanamama na Muimbaji wa nyimbo za zouk na R&B toka Tanzania,Stara Thomas kwa sasa amempa Bwana Yesu maisha yake
Mwanamama huyo alishawahi kutamba nyimbo kama Niko kwa ajili yako,Nakupenda , Na Nyingine nyingi Pia alishawahi kufanya kazi za pamoja na wasanii wenziwe kama Mh Mbunge wa Mbeya Mjini Mr 2 aka Sugu katika wimbo ulijulikana kama Sugu,Riziki ya K Basil, Nipigie na AT hata Chidi Benz..Kwa mujibu wa wa chanzo cha habari hizi mwanamama Huyo alisikika akisema
“Nilipata wito kutoka kwa Yesu kwa kuwa aliwaita watu wote wasumbukao na kulemewa na mizigo waende kwake atawapumzisha” Stara ambaye kwa sasa anaabudu kanisa la Shalom lililoko Mbezi-Salasala....Na atakua amefuata nyayo za Wasanii wengine Renee Lamira,K-Basil na wengine wengi.
“Nilipata wito kutoka kwa Yesu kwa kuwa aliwaita watu wote wasumbukao na kulemewa na mizigo waende kwake atawapumzisha” Stara ambaye kwa sasa anaabudu kanisa la Shalom lililoko Mbezi-Salasala....Na atakua amefuata nyayo za Wasanii wengine Renee Lamira,K-Basil na wengine wengi.








