Neno ‘chakachua” tangu liingie,limekuwa likitumika kuelezea takribani kila kitu ambacho hakiendi sawa.Ilikuwa ni suala la kusubiri tu kabla ya msanii fulani hajalitumia neno hilo katika wimbo au kuupa wimbo jina hilo.
Naam,hakuna haja ya kuendelea kusubiri kwani yupo msanii mpya ambaye ameamua kuingia na wimbo unaokwenda kwa jina hilo.Msanii huyu mpya anaitwa Ochu Eddy Sheggy.Yes,ni mtoto wa Marehemu Eddy Sheggy yule mwimbaji mahiri wa muziki wa dansi aliyewahi kutamba sana.
Wimbo huu umetengenezwa katika studio mpya za Seductive Records chini ya Producer Jilly Baby.Video ya wimbo huu ambayo tayari imeshaanza kusambazwa katika vituo mbalimbali vya TV imetengenezwa na EmptySoulz Production.Usikilize wimbo huo hapo chini.Ni ladha nzuri ya Zouk.
Naam,hakuna haja ya kuendelea kusubiri kwani yupo msanii mpya ambaye ameamua kuingia na wimbo unaokwenda kwa jina hilo.Msanii huyu mpya anaitwa Ochu Eddy Sheggy.Yes,ni mtoto wa Marehemu Eddy Sheggy yule mwimbaji mahiri wa muziki wa dansi aliyewahi kutamba sana.
Wimbo huu umetengenezwa katika studio mpya za Seductive Records chini ya Producer Jilly Baby.Video ya wimbo huu ambayo tayari imeshaanza kusambazwa katika vituo mbalimbali vya TV imetengenezwa na EmptySoulz Production.Usikilize wimbo huo hapo chini.Ni ladha nzuri ya Zouk.








