Google PlusRSS FeedEmail

BABY MADAHA AJIVUNIA KUTUNGA MISTARI AKIWA MTUPU



MSANII wa kike anayetamba kwenye gemu la muziki wa bongo fleva Baby Madaha anajikuta nafungua mwaka na kituko cha aina yake kwa kupenda kukaa utupu bila ya kuvaa chochote pindi awapo nyumbani kwake

Nyota huyo ambaye anajikuta kupenda kukaa utupu siku nzima awapo nyumbani kwake bila ya kuvaa nguo yoyote ile hali hiyo inampa ugumu sana pindi anapotembelewa na wageni nyumbani kwake

Mwenyewe anabainisha kuwa anapata mawazo ya nyimbo mpya akiwa na hali hiyo ya kutovaa nguo, na kuweza kuandika mistari ya nyimbo akiwa katika hali ya utupu

Akiwa bafuni pia ndio muda wake mzuri kwake wa kuendelea kushuka mistari, hivyo bafuni huko anakutumia kwa ajili ya kuogoa na kutunga mistari yake kadhaa ya nyimbo zake

"Ninapenda sana kukaa uchi huku nikiwa naandika mistari ya nyimbo pia ninapokuwa bafuni ndipo muda wangu wa kushuka mistari yaani hali ya kukaa utupu ndio inanisababisha niweze kutunga mistari kwa wingi" alisema Baby Madaha

Hicho ndio kituko cha Baby Madaha ambaye anajikuta akitunga mistari akiwa bafuni huku hali ya kukaa utupu ikimwezesha kupata kilicho bora zaidi katika muziki wake





Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging