ADELE KUNUNULIA FAMILIA GHOROFA
Mwanamuziki Adele ameripotiwa kutangaza dau la kununua jumba la kifahari kwa ajili ya ndugu zake, muimbaji huyo wa kibao cha The 'SkyFall' anasema kuwa mara kadhaa alikuwa akipanga kununua mjengo huo lakini akawa anahairisha
Vyanzo vya habari vilivyopo karibu na mwanamuziki huyo vilieleza kuwa Adele kwa sasa anataka kuifurahisha familia yake kutokana na mafanikio aliyoyapata, vyanzo hivyo vilieleza kuwa mwanamuziki huyo anataka kununua jumba lenye gorofa saba lililopo jijini London karibu na anapoishi