BILL ASAMOAH AUMIZWA NA KSHFA YA USHOGA
Mwigizaji Bill Asamoah amewajia juu watu wanaosema yeye ni shoga kutokana na kuigiza filamu ya ushoga na kueleza kuwa hatamani hata kutembea kutokana na kuzongwa na watu hasa wanawake wakimwita shoga
Kauli hiyo ya mugizaji huyo maarufu nchini Ghana imekuja baada ya kucheza filamu ya 'Ampre Bre' ambayo ilikuwa ikimuonyesha athari za ushoga na badala yake imepokelea kwa mtazamo wa tofauti na jamii kiasi cha kumfanya asiwe na raha hata ya kutembea
Alifafanua kuwa ni ngumu kuwaeleza watu wote kuwa alikuwa anaigiza hasa wale wasioelewa kwa kuwa baadhi yao wanaelewa na kujua ile ni kazi na wala siyo ukweli