DEANNA DURBIN AFARIKI DUNIA
Mwanamuziki nyota na muigizaji wa zamani Deanna Durbin amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 91, mwanamuziki huyo ambaye pia ni muigizaji aliyekuwa akilipwa fedha nyingi akiwa na umri mdogo miaka ya 1930 alifariki nchini kwao Canada
Mtoto wake wa kiume aitwaye Peter David aliliambia gazeti la Deanna Durbin Society kwamba mama yake alifariki siku kadhaa zilizopita lakini hakutoa maelezo zaidi
Mwisho mwa miaka ya 1930, Durbin alivuma sana baada ya kutokea kwenye filamu nyingi za vichekesho jambo ambalo lilifanya atunukiwe tuzo nyingi