Google PlusRSS FeedEmail

JAY Z AZUNGUMZIA UZUSHI KUHUSU UJAUZITO WA MKEWE BEYONCE

Baada ya kusambaa kwa uvumi kuwa mkewe Beyonce ni mjamzito kwa takribani miezi miwili sasa uvumi huo bado ukizidi  kuendelea.! 
Jay-Z ameweka bayana kuhusu swala hilo alipo kuwa anahojiwa na kituo kimoja cha redio nchini Marekani amesema uvumi huo so wa kweli mkwe si mjamzito..
Nguli huyo wa Hip hop na mjasiriamali mkubwa aliongeza kwa kusema .” Najua watu wanajua nimeoa lakini sipendi kuzungumzia maisha yangu binafsi hazarani kwasababu yananihusu mimi binafsi na jibu naloweza sema ni HAPANA  hakuna ujauzito wowote, nashangaa watu wanazusha vitu tu na wakati mama yangu yupo nayeye ndio angekuwa wa kwanza kujua”
Alipoulizwa juu ya maoni ya rafiki wake wa karibu Kanye West aliyoyatoa kwa Rais wa zamani wa nchi hiyo George Bush kuwa ni mbagauzi alijibu. Ilikuwa mbaya kwa muda ule lakini zilikuwa hisia za kweli. Sisi kama watu weusi hatukuona  janga la  Katrina ni la  kiasili bali lilikuwa shambulio  kwa watu weusi.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging