Mmoja wa Artist anayeunda kundi la Watengwa toka Kijenge ya juu pande za A-Town,Pacha Izz ameuwawa kwa kuchomwa kisu. Kwa mujibu wa Jacob Makala aka Rapper JCB toka Kundi la Watengwa,tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana pande za Clock Tower pale City Center na kulitokea kupishana kiswahili na Changudoa akitokea Club,Na baada ya kufanya tukio hilo Dada huyo alikamatwa na kupelelekwa Polisi na Mama mzazi wa Marehemu Pacha Izz aliomba huyo dada aachiwe! Kwa sasa mipango ya mazishi bado inafanywa na hajajulikana Pacha Izz atazikwa lini.Na tukio hili linafanana na lile la kuchomwa kisu kwa Hip-Hop Artist toka kundi la X-Plastaz,Marehemu Chrizostorm Buchard aka Faza Nelly,March 26 2006 jijini Arusha na kichaa toka pande hizo.
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.