
Mwanamuziki gwiji wa Soul , Sylvester Sterwar aka Sly Stone ,ambaye alishawahi kutamba miaka ya 1960 hadi 1970 anaishi ndani ya gari na hajui hatima ya maisha yake

Kwa mujibu wa Tmz imesema kuwa sly stone 68 ambaye aliwahi kufungwa baada ya kukamatwa na dawa za kulevya,amepoteza matumaini baada ya kufilisika kutokana na maisha ya anasa,ulevi na matumizi mabaya ya fedha..Hali ya sly stone aliyewahi kumiliki jumba la kifahari katika kitongoji cha Beverly Hills,wakati bendi yake ya Sly And The Family Stone,ilipata umaharufu mkubwa na kupanda chati na vibao vyake kikiwemo kibao chake Dance To The Music..







