
“Katika filamu zangu hii ni nzuri kupita maelezo, na nimetayarisha mwenyewe kwa kushirikiana na ndugu yangu katika kutengeneza, kwa sasa nimejitoa kufanya kazi kwa nguvu zaidi na kwenda mbele katika tasnia ya filamu nyumbani, Dr. Thomas ni filamu ya aina yake,” analonga Love.
Mwanadada anayekuja juu katika tasnia ya filamu Tanzania Loveness Watson anatarajia kuachia filamu mpya inayokwenda kwa jina la Dr. Thomas, filamu hiyo ipo tayari kwa ajili ya kusambazwa na itasambazwa nchi nzima ili kila mpenda filamu waione.







