Google PlusRSS FeedEmail

GANGWE MOB WAJITOA KATIKA UZINDUZI WA ANTI VIRUS-WATAPANDA STAGE MOJA NA DMX NA FABOLOUS

Wakati ndio kwanza wadau wakiwa macho na hamu ya kusubiri show kubwa ya Vinega,ili kuzindua Anti Virus ,mambo si mazuri kwa upande huo,Pro-24 imepata taharifa kwaba vijana wa Gangwe Mob hawatashiriki katika show hiyo ambayo inatarajiwa kufanyika Nov 26 katika viwanja vya Posta Kijitonyama Jijini Dar es Salaam.Gangwe Mob ikiwa inaundwa na Inspector Harun na Luten Kalama. Pro-24 ikaamua kukutana na wasanii husika na kuzungumza ili kupata ukweli wa jambo hilo,Inspector alisema"ni kweli sisi kama Gangwe Mob Hatutashiriki katika show ya Vinega kutokana na Longolongo katika swala zima la malipo,waandaaji wanasema tutalipwa baada ya kupatikana viingilio mlangoni show isipolipa ina maana hakuna kitakacholipwa ila Tumepata kazi Nov 26 tutakuwa Leders Club kwenye show ya Dmx na Fabolous.Ila kimuonekano mara baada ya kuzungumza nao inaonekana Kalama bado ana nia ya kushiriki katika show ya vinega nini kitafata endelea kufatilia...

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging