Google PlusRSS FeedEmail

DR CHENI HUYOO KWENYE KOMEDI

Mahsein Awadh ‘Dr. Cheni’ amebadirika na kuingia katika uchekeshaji na kuigiza huku akiwa mhusika mkuu katika komedi aliyoipatia jina la Dr. Kifimbo ni kitu tofauti sana kwa muigizaji wa filamu kuigiza kuchekesha na kumudu kwani wengine wanafahamu kuwa uchekeshaji ni fani ngumu..“Ni komedi inayokuja kufanya mapinduzi katika Ulimwengu wa Komedi tunapomuongelea huyu Dr. Kifimbo yeye anadili na wagonjwa wenye magonjwa ya kujitakia, kwa mfano mtu anapoumwa magonjwa kama vidonda vya tumbo sababu yake ni kushinda bila kula na kuwa na njaa dawa ninayotoa hapa ni viboko tu,”anasema Dr. Cheni. Kwa kupitia kampuni yake ya Dr. Cheni Creation Arts ameandaa komedi nyingine inayokwenda kwa jina la Old is Gold anayoshirikiana na wasanii wa Komedi Wakongwe kama Mzee Onyango, Mwita Maranya, Mahoka kutoka Zanzibar, Pembe, Senga, Zimwi, Mboto, Samofi na wasanii wengine wengi waliotamba siku za nyuma.

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging