Google PlusRSS FeedEmail

MATUKIO YA SHOW YA DIAMOND ARE FOREVER


 Msanii wa Muziki wa kizazi kipya Ommy Dimpozzz akifanyiwa mahojiano mara baada ya kuwasili kwenye tamasha la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Diamond Platinum akiwarusha mashabiki waliohudhuria katika tamasha lake la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Diamond akionyesha umahili wake wa kuimba.
 Janeth Sostenes akifanya mahojiano na Godwin Gondwe.
Madansa wa Diamond wakiwajibika nae
Mashabiki wa kutosha wakifuatilia show.


Utata ulianzia hapa pale Dimond alishuka stejini na kwenda kwenye meza waliokuwa wamekaa akina Steve Nyerere na Mboni Masimba na ndipo alipopewa t-shirt ambayo kwa mujibu wa udadisi na uchunguzi wa udadavuzi wa mambo wa Kajuna Blog, ilisemekana kuwa t-shirt hiyo ilikuwa inapicha ya mwanadada ambaye alikuwa akitoa na Diamond kwa sasa. Na ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kumrusha roho Wema Sepetu.
Mwanadada Mboni Masimba akimkabidhi Diamond t-shirt huku Steve Nyerere akimtunza, vile vile alichukua t-shirt aliyopewa na kuipeleka kwa mwanadada Jokate Mwegelo.
  Hapa akikabidhiwa t-shirt na kupewa maelekezo mahali pa kuipeleka.
Baada ya hapo kumaliza lile movie la kwanza aliendelea na kupita katika meza mbali mbali huku akiwasalimia wageni waalikwa.
...Akiimba na bendi ya Odama ambayo alimpa ushirikia mkubwa.

Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya Q-chief akimpa sapoti mdogo wake Diamond

Ehe! utata mkubwa ambao ulizuka ni hapa ambapo mwanadada huyu alimtuza dola za Kimarekani, Diamond
Diamond aliendelea kuimba huku mwanadada huyo akimtunza huku akitoa tabasamu na kicheko

Mwadada huyo hapa alikuwa amemaliza na kuondoka kwa mikogo..






Hapa wema akiondoka kwenye Stage mara baada ya kumtunza Diamond ambapo fedha zake hazikupokelewa na msanii huyo

Shamim Mwasha akilaumu kitendo alichokifanya Diamond cha kukataa hela alizoenda kutuzwa na Wema... 'Haiwezekani hii ni aibu sana'

Pesa alizokataa  kuzichukua Diamond  zikiwa kwenye stage

Hapa alipiga kitu cha 'Nimpende Nani'

Jokate na marafiki zake wakishangilia


Diamond alishuka na kuelekea kwa mwanadada Jokate Mwegelo na kuanza kukata mauno.Pembeni mwanadada Mboni Masimba akiwa amevaa t-shirt alizokuwa amevaa.

Aha! nimependeza sana
Taji Liundi akimbembeleza Diamond ili aende nae kwa Wema ili akaombe msamaha kwa kitendo kilichotokea ndipo Diamond akakataa.

Mwanadada Mariam (Miss Popular) akimfuta jasho Diamond wakati Taji Liundi akimbembeleza ili aende kwa Wema.

 

wema akiliwanzwa na marafiki zake mara baada ya kutoa fedha na kutochukuliwa na Diamond


Hapa akizidi kulia na mashosti zake wakimliwaza

Msanii wa kizazi kipya, Ommy Dimpozzz akimpa sapoti Diamond...huku akitoa ushuhuda wa maisha yake na ya Diamond walipotoka.

...baada ya ujumbe wa Ommy Dimpozz, Diamond alimwaga chozi na hapa alikuwa akijifuta.

Amini nae hakuwa nyuma kumpa sapoti

Barnaba, Amini na Diamond wakiwajibia

This entry was posted in

Leave a Reply

    Powered By Blogger

    Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below...

    Get This SpiceUpBlogging