Mwigizaji wa kike katika tasnia ya filamu Loveness Watson ‘Love’ amemlalamikia shoga yake wa karibu kwa kumkatia buzi lake kamba baada ya kumfanyia vitina kwa kumpigia simu na kumweleza umbeya kuhusu kuwa na uhusiano na king’asiti aliyetajwa kwa jina moja la George Love amemtaja shoga yake kwa jina la Theopista Reverian ‘Dina’.Love anasema kuwa rafiki yake huyo alimpigia simu mchumba wake huyo baada ya kuchukua namba ya simu ya mpenzi“Yaani huyu shoga yangu Dina hana shukrani kabisa kwani yeye hana kampani kama mimi kwa hiyo kila nikiitwa katika filamu lazima nimchukue kwa sababu ni rafiki yangu lakini ameniharibia kwa Mchumba wangu tena wakati ambao nilikuwa na mipango mikubwa sitaki tena shoga, maana huyu Dina alichonifanya sitamsahau,”anasema Love.Kwa huyo ambaye hakutaka kumtaja jina kutokana na wadhifa wake katika jamii, alipompigia simu na kumweleza kama yeye ni msichana asiye mwaminifu kwani ana mahusiano na wavulana wengi, jambo lilomfanya bwana huyo kusitisha uhusiano na kukataa kutoa mtaji wa filamu zaidi ya milioni siti alizomwahidi.
PRO24 RADIO/TV
CLICK AND ENJOY GOOD MUSIC
MIXTAPES
ARTIST PROFILES
Blog Archive
LOVE LINKS
PRO-24 DJS OFFICIAL BLOG
PRO24 ENTERPRISES. Powered by Blogger.








